Serengeti Boys yaendelea kujifua fainali za vijana

0
1220

Kocha mkuu wa timu ya taifa ya vijana wenye umri chini ya miaka 17, Serengeti boys – Oscar Mirambo amesema katika kipindi kifupi kilichobaki kuelekea fainali za afrika kwa vijana wa umri huo watapambana kupata michezo ya kimataifa ya kirafiki na timu kutoka magharibi mwa bara la Afrika.

Mirambo anasema anaamini michezo ya kimataifa ya kirafiki na mataifa hayo itawajenga zaidi vijana wake kutokana na utimamu wa mwili waliokuwa nao vijana wa mataifa hayo ambayo kwa kiasi kikubwa yamekuwa yakisumbua kwenye soka la Afrika.

Kwa upande wao nahodha wa kikosi hicho Morice Abraham na mshambuliaji machachari Kelvin John wamesema wapo tayari kwa fainali hizo na watapambana kuhakikisha kombe linabaki hapa nchini.

Serengeti boys wamepangwa kundi Aa kwenye fainali za kombe la mataifa ya Afrika kwa vijana wenye umri chini ya miaka 17 pamoja na mataifa ya Nigeria, Angola na Uganda wanaoshiriki kwa mara ya kwanza fainali hizi, huku kundi Be likiwa na timu za Guinea, Cameroon, Morocco na Senegal.

Vijana wa Serengeti Boys wataanza kampeni ya kusaka taji kwa kuumana na Nigeria, Aprili 14 katika dimba la TaifA jijini dsm kwenye mchezo wa ufunguzi.

Michuano hiyo itadumu kwa wiki Mbili kuanzia aprili 14 hadi 28 katika viwanja vitatu vya jijini dsm, ambavyo ni uhuru, taifa na azam complex.