Mtibwa wajipanga kuwadhibiti KCCA ya Uganda Disemba 22

0
1200

Kocha mkuu wa Mtibwa  Sugar, Zuber  Katwila amesema anatambua kibarua walichonacho cha kupindua matokeo mbele ya Kcca ya Uganda kwenye mchezo wa marudiano wa kombe la shirikisho barani Afrika utakaochezwa kwenye dimba la Chamazi, lakini amekiandaa vyema kikosi chake  kwa ajili  ya kupambana na kuibuka na ushindi.

“Kikosi change kipo imara kupigania matokeo ya ushindi  kwenye mchezo huo na kwamba tutaingia na tahadhari kubwa kutokana na ubora wa wapinzani wetu na kwamba tutatumia kucheza  soka la kushambulia zaidi”alisema katwila

Mtibwa sugar wanahitaji ushindi wa mabao manne kwa bila mbele ya Kcca, ili waweze kusonga mbele katika hatua inayofuata ya michuano hiyo kufuatia kula mweleka wa mabao matatu kwa bila katika mchezo wa kwanza uliochezwa jijini Kampala nchini Uganda.

Mchezo huu utatangazwa mubashara na tbc taifa kuanzia saa kumi alasiri.

Katika michezo mingine ya kombe la shirikisho vita kubwa itakuwa kati ya Elgeco Plus  alfa ya madagascar wataalika kaizer chiefs ya afrika kusini katika mchezo ambao wanahitaji ushindi wa mabao manne kwa bila ili kusonga mbele.

Daring club Motema Pembe ya Jamhuri ya kidemokrasi ya Congo watakuwa wageni wa fc san Pedro ya Ivory Coast baada ya sare ya bao moja kwa moja katika mchezo wa kwanza huku salimata et tasere fc ya burkina faso wakiwa na faida ya ushindi wa mabao mawili kwa bila walioupata kwenye mchezo wa kwanza uliochezwa juma moja lililopita nchini misri watawaalika wabaya wa simba, Al Masry ya Misri huku asante kotoko ya ghana baada ya matokeo ya suluhu ugenini juma lililopita, watakuwa wenyeji wa kariobangi sharks ya kenya.