Pluijm ajiuzulu ukocha Singida BS

0
337

Kocha Mkuu wa Singida BS, Hans Van der Pluijm amejiuzulu nafasi hiyo baada ya kuitumikia tangu mwaka 2022.

Kufuatia uamuzi huo walima alizeti hao wa Singida watakuwa chini ya Kocha Msaidizi, Mathias Lule mpaka pale itakapoamuliwa vinginevyo.

Kwa mujibu wa taarifa ya Singida BS, kocha huyo amejiuzulu kwa kile alichoeleza kuwa anahitaji muda zaidi kwa ajili ya masuala yake binafsi.

Kocha huyo amekuwa na mafanikio makubwa ambapo aliiwezesha timu kumaliza nafasi ya nne katika ligi, kufuzu Kombe la Shirikisho Afrika na hivi karibuni amewezesha kusonge mbele kwenye mashindano hayo ya Afrika baada ya kuvuka mzunguko wa kwanza.