Manchester city yairarua Burton Albion mabao 9 kwa bila

0
870

Timu ya Manchester City imetanguliza mguu mmoja katika fainali ya michuano ya kombe la ligi pale England lijulikanalo kama  Carabao baada ya kuifunga timu ya Burton Albion mabao Tisa kwa bila.

Mabao Manne ya Gabriel Jesus, na mengine yaliyofungwa na Kevin De bruyne, Oleksandr Zinchenko, Phil Foden, Kyle Walker na Riyad Mahrez yametosha kuandikisha rekodi mpya kwa Manchester City kupata ushindi mnono wa mabao zaidi ya nane baada ya miaka 31, kwani mara ya mwisho walipata ushindi mnono kwa kuinyuka Huddersfield Town mabao kumi kwa bila, novemba 1987.

Manchester City sasa wanaandika pia rekodi ya kufunga mabao 16 ndani ya siku nne baada ya jumapili iliyopita kuibuka na ushindi wa mabao saba kwa bila dhidi ya Rotherham United katika mchezo wa mzunguko wa tatu wa kombe la Fa.

Manchester city sasa watakuwa na kazi rahisi kuelekea mchezo wa marejeano dhidi ya Burton Albion utakaochezwa januari 23katika dimba la Pirelli,  ambapo mshindi wa jumla ataungana na mshindi wa jumla wa mchezo kati ya Chelsea na Tottenham Hotspur kufuzu kwa hatua ya fainali.

Tottenham wanafaida ya bao moja walilolipata katika ushindi mwembamba wa bao moja kwa bila walioupata katika mchezo dhidi ya Chelsea.

Fainali ya michuano hii itafanyika februari 24 katika dimba la wembley mjini London.