United yaichapa Newcastle, yakwea hadi nafasi ya pili EPL

0
120

Timu ya Manchester United imeibuka na ushindi wa 3-1 dhidi ya Newcastle United katika mchezo wa Ligi Kuu ya England uliopigwa usiku wa jana, katika Uwanja wa Old Trafford.

Mabao ya Manchester Unted yamefungwa na Marcus Rashford dakika ya 30, Daniel James dakika ya 57 na Bruno Fernandes kwa penalti dakika ya 75, wakati bao la Newcastle United limefungwa na Allan Saint-Maximin dakika ya 36.

Kwa ushindi huo, Manchester United inafikisha pointi 49 na kurejea nafasi ya pili,ikiizidi wastani wa mabao tu Leicester City, wote wakiwa nyuma ya Manchester City inayoontoza kwa pointi 10 zaidi baada ya kwote ucheza mechi 25