Simona ashindwa kumfunga Barty katika mchezo wa tenes

0
925

Mchezaji namba moja kwa ubora wa tesniss duniani kwa upande wa kinadada  Simona Halep  ameshindwa kutamba mbele ya   Ashleigh Barty wa Australia katika michuano ya  Kimataifa ya Sydney.

Mromania huyo ambaye alikuwa nje ya mchezo huo kwa takribani miezi mitatu kutokana na kuwa majeruhi amenyukwa seti mbili kwa bila kwa matokeo ya seti  6-4 na  6-4 na Barty ambaye ni mchezaji namba 15 kwa ubora duniani.

Halep mwenye umri wa miaka 27 ambaye ni bingwa wa mashindano ya wazi ya Ufaransa, ameanza mashindano hayo bila ya kocha wake huku pia akitarajia kushiriki mashindano makubwa ya teniss ya wazi ya Australia hivi karibuni.