Simba yarejea Dar es salaam kujiandaa na mchezo dhidi ya Saoura ya Nigeria

0
946

Kikosi cha Simba kinarejea leo kutoka Zanzibar kilipokuwa kinashiriki kombe la Mapinduzi tayari kujiandaa na mchezo wa ligi ya mabingwa Afrika dhidi ya Saoura ya Algeria mchezo utakaochezwa katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam Januari 12.

Katika mchezo wa Januari 8,Simba ilifunga timu ya Mlandege kwa  bao moja kwa bila na kutinga hatua ya nusu fainali ya michuano hiyo ambapo kikosi cha pili cha Simba kitacheza mchezo huo.

Bao pekee la Simba lilifungwa na Haruna Niyonzima kwa mkwaju wa penati baada ya beki wa pembeni wa Simba Asante Kwasi kuangushwa katika eneo la penati.

Matokeo ya michezo  mwingine uliochezwa  jana timu ya Kmkm imeibuka  na  ushindi wa mabao matatu kwa bila dhidi yaK,na kuifanya Kmkm kucheza hatua ya nusu fainali ya michuano hiyo.

Michezo hiyo ya kombe la Mapinduzi inaendeleo kwa kuzikutanisha mabingwa watetezi wa michuano hiyo Azam Fc dhidi ya Malindi.