Pellegrini kuisaidia Man City

0
851

Kocha wa timu ya West Ham United, -Manuel Pellegrini amesema anataka kuifunga Liverpool ili kuisaidia timu yake ya zamani ya Manchester City kwenye harakati za kuusaka ubingwa wa Ligi Kuu ya  England.

Februari Tatu mwaka huu, Manchester City iliifunga Arsenal na hivyo kupunguza pengo la alama kufikia mbili  dhidi ya Liverpool huku Liverpool wakiwa na mchezo mmoja mkononi dhidi West Ham United.

Pellegrini raia wa Chile alishinda ubingwa wa England mwaka 2014 akiwa kocha wa Manchester City na amesema kuwa kama wakishinda itakua ndio furaha yake.

West Ham United ipo katika nafasi ya 12 kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya England na katika mchezo wake wa hivi karibuni itamkosa mlinzi wake Winston Reid ambaye anauguza jeraha la goti kwa muda wa mwaka mmoja.