Kocha wa Manchester City ajitapa kunyakua ubingwa wa England

0
1213

Kocha wa Manchester City, Pep Guardiola amesema kikosi chake lazima kikubali kuwa wapinzani wao kwenye mbio za kuwania ubingwa wa Ligi Kuu ya England, Liverpool huenda ndiyo timu bora kwa sasa duniani.

Mabingwa hao watetezi ambao jana wameibuka na ushindi wa mabao matatu kwa moja dhidi ya Southampton alhamisi wiki hii wanakabiliwa na kibarua kigumu cha kumenyana na vinara Liverpool kwenye Dimba la Etihad huku tofauti ya alama baina yao ikiwa ni alama saba.

Kuelekea mchezo huo Guardiola anasema tatizo ni kwamba wapinzani wao wapo kwenye ubora wa hali ya juu na wanaweza kuwa ni timu bora kwa sasa Barani Ulaya na hata duniani.

Wakati Manchestr City wakipokea vipigo kutoka kwa Chelsea, Crystal Palace na Leicester City Liverpool wao wameshinda mechi zao zote saba walizocheza na wamemaliza mwaka 2018 kwa kugawa dozi nzito baada ya kuitandika Arsenal mabao matano kwa moja.