JKT Queens yatwaa ubingwa wa CECAFA

0
299

Timu ya JKT Queens kutoka Tanzania imeshinda ubingwa Ligi ya Mabingwa ya CECAFA kwa Wanawake baada ya kuifunga CBE Women ya Ethiopia kwa mikwaju ya penati.

Miamba hiyo ilikwenda dakika 120 bila kufungana na hivyo mikwaju ya penati ikaamuliwa kama njia ya kumpata bingwa ambapo JKT Queens imeshinda kwa penati 5-4.

Kufuatia ushindi huo, JKT Queens ndio itakayouwakilisha ukanda wa CECAFA kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa ya CAF kwa Wanawake.

Mashindano hayo yatafanyika Novemba 2023 nchini Ivory Coast.