Waziri Mkuu aongoza mazishi ya kitaifa waliokufa ajali ya MV Nyerere

0
2249

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ameongoza wananchi katika mazishi ya kitaifa ya watu waliofariki dunia kwenye ajali ya MV Nyerere iliyotokea Septemba 20, mwaka huu.

Akizungumza katika mazishi hayo yaliyofanyika katika eneo la Bwisya, kisiwa cha Ukara wilaya ya Ukerewe mkoani Mwanza Waziri Mkuu amesema serikali imeanza kuchukua hatua kwa wale wote wanaohusika na shughuli za kivuko hicho wakati uchunguzi wa chanzo cha ajali hiyo ukiendelea.

Waziri Mkuu amesema serikali imechukua hatua ya kuunda tume ya uchunguzi na kuahidi tume hiyo kutangazwa wakati wowote.

Ili kukabiliana na tatizo la usafiri lililopo, Waziri Mkuu amesema meli ya MV Nyehunge imeanza kutoa huduma ya usafiri wa muda badala ya MV Nyerere iliyokuwa ikitoa huduma kati ya bandari ndogo ya Bugolora, Ukerewe na kisiwa kidogo cha Ukara.