Rais Magufuli avunja bodi TEMESA

0
2397

Kufuatia ajali ya kuzama kwa kivuko cha MV Nyerere iliyotokea tarehe 20 Septemba, 2018 katika ziwa Victoria, Rais Dkt. John Magufuli ameivunja Bodi ya Ushauri ya Wakala wa Ufundi na Umeme -TEMESA.

Bodi hiyo iliyo chini ya Mwenyekiti wake Brigedia Jenerali Mstaafu Mhandisi Mabula Mashauri imevunjwa kuanzia leo tarehe 23 Septemba wakati kamati ya uchunguzi kwa kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama vikiendelea na uchunguzi wa ajali hiyo.