Tume ya ushindani nchini kufungua ofisi kila kanda

0
1167

Tume ya Ushindani Nchini – FCC – imeweka mikakati ya kufungua ofisi zake kila kanda ili kusimamia kwa ukaribu ushindani wa bidhaa zinazozalishwa na kuingizwa hapa nchini ili kumlinda mlaji.

Mkurugenzi wa FCC Dkt. John Mduma amesema hayo mkoani Mtwara katika semina kuhusu sheria ya ushindani kwa wajumbe wa kamati ya ushauri ya mkoa.

 Amesema ili kuhakikisha Tume inafanya vizuri imeweka mikakati ya kufungua ofisi kila kanda ili kusimamia kwa ukaribu ushindani wa bidhaa zinazozalishwa na zinazoingizwa hapa nchini ili kumlinda mlaji.

Tume ya ushindani kwa sasa inafanya uchunguzi kwa wafanyabiashara na wamiliki wa kampuni zinazozalisha bidhaa zinazofanana ambao wana mpango wa kutopeleka bidhaa sokoni kwa lengo la kuharibu ushindani.