Wamiliki wa maabara kufuata taratibu za usajili

0
1177

Mkurugenzi wa Huduma za Tiba kutoka Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Dkt. Dorothy Gwajima amewataka wamiliki wa maabara binafsi za afya kufuata utaratibu wa kusajiliwa na kutambuliwa kisheria.

Akizungumza jijini Dar Es Salaam na waandishi wa habari Dkt. Gwajima amesema wamiliki wa maabara ambao hawatimiza matakwa ya kisheria watafungiwa na kushtakiwa kwa mujibu wa sheria.

Amesema wizara hiyo inashirikiana na viongozi wa serikali kuu na serikali za mitaa ili kubaini maabara zinazokiuka taratibu na sheria.

Mpaka sasa ni asilimia 58 za maabara binafsi zilizopo nchini ndizo zinatekeleza matakwa ya kisheria.