Tanzania na Kuwait kuimarisha ushirikiano

0
2173

Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan amekutana na kufanya mazungumza na Balozi mpya wa Kuwait nchini Mubarak Mohammed Faleh Alsehaijan.

Balozi Alsehaijan alifika ofisini kwa Makamu wa Rais jijini Dodoma kwa lengo la kujitambulisha.

Wakati wa mazungumzo yao, viongozi hao wamesisitiza kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na Kuwait kwa manufaa ya nchi zote mbili na watu wake.