Waliotekwa Cameroon waachiliwa

0
2201

Waasi nchini Cameroon wameliachia kundi la wanafunzi 74 waliowatekwa wakiwa shuleni Novemba tano mwaka huu.

Mbali na wanafunzi hao, watu wengine waliotekwa na waasi hao ni walimu kadhaa waliokuwa wakiwafundisha wanafunzi hao pamoja na dereva wa basi la shule.

Kasisi mmoja wa kanisa Katoliki nchini Cameroon aliyekuwa akisimamia mazungumzo kati ya waasi hao na serikali, mazungumzo yaliyosaidia kuchiliwa kwa wanafunzi hao amesema kuwa bado waasi hao wanamshikilia mkuu wa shule na mwalimu mmoja wa shule ya sekondari wanaposoma wanafunzi hao.