RAIS SAMIA AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA BARABARA RUANGWA – NANGANGA

0
151

Rais Samia Suluhu Hassan ameweka jiwe la Msingi la ujenzi wa barabara ya Nachingwea – Ruangwa – Nanganga, sehemu ya Ruangwa – Nanganga yenye urefu wa kilomita 53.2 inayojengwa kwa kiwango cha lami ambapo hadi kukamilika kwake itagharimu shilingi Bilioni 50.3.

Akizindua ujenzi wa barabara hiyo Rais Samia amesema Serikali imejipanga kujenga miundombinu ya mikoa ya Kusini ili kurahisisha usafirshaji wa mazao na kukuza uchumi wa mikoa hiyo na hivyo kuwataka Wakandarasi wakamilishe ujenzi wa barabara hiyo kwa wakati.

“Niwaombe wakandarasi na wasimamizi waende kwa kasi sana, lakini nipongeze TANROADS mkandarasi na wengine kwa hatua ambayo imeshafikia na kwetu sisi Serikali mafedha yapo tunasubiri certificate [cheti] ziletwe tulipe kazi ziendelee”. amesema Rais Samia

Ameongeza kuwa lengo la Serikali ni kuunganisha mkoa wote wa Lindi kwa barabara za kiwango cha lami pamoja na wilaya kwa wilaya ziunganike kwa barabara za lami.