Mwigulu: Changamoto ya upatikanaji wa dola inatatuliwa

0
276

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Nchemba amesema mipango ya Serikali katika kupunguza athari na changamoto za upatikanaji wa fedha za kigeni ni pamoja na kuimarisha sheria, kanuni na miongozo ya usimamizi na kuongeza kiwango cha kuuza fedha za kigeni katika soko la pesa za kigeni.

Amesema kati ya Machi 2022 na Agosti 2023 Benki Kuu ya Tanzania iliuza zaidi a Dola Milioni 500 za Kimarekani.

“Serikali inaendelea kuchukua hatua mbalimbali za muda mfupi na mrefu katika kukabiliana na changamoto ya upatikanaji wa pesa za kigeni hasa dola za Kimarekani hapa nchini”. amesema
Waziri Nchemba

Ametoa kauli hiyo Bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge Era Chiwelesa aliyeuliza kuhusu mpango wa Serikali katika kunusuru uchumi wa nchi kutokana na ukosefu wa fedha za kigeni hususani Dola za Kimarekani.