Wajawazito wanaokunywa pombe washtakiwe

0
145

Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii wa Afrika Kusini, Hendrietta Bogopane-Zulu amesema,
Wajawazito wanaokunywa pombe wanapaswa kushtakiwa kwa uhalifu, kutokana na pombe kuathiri ubongo wa mtoto aliye tumboni.

Akizungumza wakati wa mafunzo ya kuongeza uelewa juu ya athari za unywaji wa pombe kwa Wajawazito, Naibu Waziri Hendrietta amesema ni vema hatua hiyo ikachukuliwa kutokana na matumizi ya pombe kwa Wajawazito kuongezeka nchini Afrika Kusini.

Madhara mbalimbali yanaweza kumpata mjamzito na mtoto aliye tumboni endapo mama huyo anakunywa pombe.

Madhara hayo ni kama;

-Kuwa na kumbukumbu hafifu

-Kupata matatizo ya kuona na kusikia

-Kupata matatizo ya moyo, figo na mifupa

-Kuwa na uwezo mdogo wa kuelewa

Je! Una ushauri gani kwa wajawazito kuhusu matumizi ya pombe?