Bakwata : Tunamuunga Mkono Rais Samia

0
132

Baraza Kuu la Waislamu wa Tanzania (BAKWATA) limesema linamuunga mkono Rais Samia Suluhu Hassan na Serikali yake yote na kuwaombea Dua ili waweze kuwa na ufanisi zaidi.

Akisoma Salamu za BAKWATA katika Baraza la Maulid Kitaifa mkoani Dodoma
Katibu Mkuu wa BAKWATA Alhaj Nuhu Mruma amesema, sababu za wao kuiunga mkono Serikali ni kutokana na juhudi kubwa inazofanya katika kuwaletea Wananchi maendeleo kwenye sekta za kiuchumi, kisiasa na kijamii pamoja na kuboresha mfumo wa vyama vingi vya siasa nchini.

“Mheshimiwa mgeni rasmi ni hivi karibuni katika kujenga demokrasia nchini, aliunda kikosi kazi maalum kilichoshughulikia masuala ya demokrasia nchini na hatimaye kuyakubali maoni mengi yaliyopendekezwa na kikosi kazi hicho na mengine yameanza kufanyiwa kazi ikiwemo ruhusa ya vyama vya siasa kufanya mikutano yao ya hadhara”. amesema Mruma

Amesema jukumu lao Viongozi wa dini ni kuendelea kuishauri Serikali, kushirikiana na Serikali katika utekelezaji wa mambo mbalimbali na kuiombea amani nchi pamoja na kuwaombea viongozi wake.