TRUMP AZIKATAA KARANTINI NEW YORK NA NEW JERSEY

0
608

Rais Donald Trump wa Marekani  ametangaza kuwa hakuna ulazima wa kuweka  karantini ya kujikinga na virusi vya Corona  mjini  New York na New Jersey badala  yake  ameelekeza  kuwa taarifa za  ushauri ziendelee kutolewa kwa wanaotaka  kusafiri ili kupunguza kusambaa  kwa  virusi  hivyo.

Trump amesema amefikia  uamuzi  huo  baada  ya mashauriano  na  watendaji wake na kusema  amekiagiza  kituo cha udhibiti  na  kuzuia  magonjwa , CDC , kutoa ushauri  kwa wasafiri utakaotekelezwa na  magavana, kwa  kushauriani na serikali  kuu.
 
Suala  la karantini lilipendekezwa na magavana akiwemo gavana wa  chama  cha  Republican Ron Desantis wa  jimbo  la Florida, ambae   alitaka  kuzuia  wasafiri  kutoka  maeneo yaliyoathirika  zaidi  kwenda  katika  majimbo  yao, Lakini  hatua  hiyo  imepingwa vikali   na viongozi  wa  majimbo  hayo yanayotajwa  kuwa  na  maambukizi makubwa, ambao  wamesema   hali  hiyo  italeta  taharuki kubwa  kwa wananchi.
 
Hadi sasa idadi ya vifo imeongezeka nchini humo  na kufikia zaidi ya elfu mbili huku idadi ya  walioambukizwa ikifikia 122,000