Hamas wadai kurusha makombora

0
2069

Wanamgambo wa Hamas kutoka Mamlaka ya Palestina wamedai kurusha makombora kuelekea nchini Israel ikiwa ni hatua ya kupinga kitendo cha nchi ya Misri kutiliana saini mkataba wa amani na Israel.

Kombora hilo lilirushwa kutoka katika Ukanda wa Gaza na kuangukia eneo la kusini mashariki mwa nchi hiyo ya Israel.

Israel nayo ilijibu mashambulio kwa kurusha makombora katika maeneo Ishirini yanayodhibitiwa na Wanamgambo hao wa Hamas na kusababisha kifo cha mtu mmoja na wengine kadhaa kujeruhiwa.