Watu 12 washikiliwa kwa tuhuma za mauaji Morogoro

0
1304

Jeshi la Polisi mkoani Morogoro linawashikilia watu 12 wanaotuhumiwa kuwa majambazi sugu wakiwemo waliohusika na mauaji ya Afisa Tarafa ya Lupilo wilayani Ulanga.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini Morogoro, Kamanda wa Jeshi hilo Wilbroad Mutafungwa amesema watuhumiwa hao walikamatwa  katika msako maalumu wa kukabiliana na uhalifu katika wilaya zote za mkoa wa Morogoro.

Aidha Kamanda Mutafungwa ametoa wito kwa wananchi kuacha kujichukulia sheria mkononi baada ya hivi karibuni kuibuka mauaji yanayosababishwa na wivu wa mapenzi.