Lindi yatakiwa kuhakiki wanufaika wa TASAF

0
1298

Mkuu wa mkoa wa Lindi Godfrey Zambi ameagiza Halmashauri za mkoa wa Lindi kuhakiki wanufaika wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii -TASAF ili kuona endapo wanufaika wa mpango huo ndio wale wenye sifa zinazotakiwa.

Zambi ameyasema hayo mjini Nachingwea alipokuwa akizungumza na wanufaika wa mpango wa kunusuru kaya maskini, baada ya kubaini miongoni mwao wengine hawana vigezo vya kunufaika na mpango huo.

Amesema wapo wazee ambao wana watoto wenye uwezo lakini watoto wao wanawakimbia wakikwepa wajibu wao na kuiachia serikali.

Mkuu wa mkoa wa Lindi amewataka wananchi kujua kuwa umaskini si sifa nzuri na kumtaka mratibu wa TASAF kumpatie taarifa ya fedha za Mfuko huo kwa kipindi cha miaka mitatu iliyopita.