Ajali yaua Sita Arusha

0
2249

Watu Sita wamekufa katika ajali ya barabarani iliyotokea kwenye eneo la Naja Mti Mmoja wilayani Monduli mkoani Arusha.

Ajali hiyo imehusisha roli lililokua lilkitoka katika kambi za wakimbizi mkoani Kigoma ambalo limegongana na gari dogo.

Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama mkoani Arusha ambaye pia ni Mkuu wa mkoa huo Mrisho Gambo amesema kuwa miili ya watu waliokufa katika ajali hiyo imehifadhiwa katika hospitali ya mkoa wa Arusha, – Mount Meru.

Majeruhi wawili wa ajali hiyo wamelazwa katika hospitali ya Seliani ambapo Gambo amewajulia hali.

Kaimu Mganga mkuu wa mkoa wa Arusha, – Omari Chande amesema kuwa amepokea miili ya watu Watano, minne ikiwa ni ya raia wa kigeni huku mmoja ukiwa ni wa Mtanzania.

Kwa upande wake Mkuu wa kitengo cha magonjwa ya dharura katika hospitali ya Seliani Dkt Peter Mabula amesema kuwa amepokea majeruhi wawili wa ajali hiyo pamoja na mtu mmoja aliyekuwa na hali mbaya ambaye baadaye alifariki dunia.