Wakazi wa Katavi walalamikia barabara zao kujengwa chini ya kiwango

0
853


Baadhi ya wakazi wa mtaa wa Makanyagio Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi wameuomba uongozi wa Mkoa huo kuingilia kati ujenzi wa miundombinu ya barabara inayodaiwa kujengwa chini ya kiwango.

Akizungumza na Tbc, Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Makanyagio, Simon Misonge amesema hali ya mtaa huo si nzuri kwa sasa kutokana na barabara kuzunguka mtaa huo kusombwa na maji ya mvua zinazoendelea kunyesha kutokana na kukosekana kwa mitaro madhubuti ya kuhimili maji.

Kila kona ya Mtaa wa Makanyagio umezungukwa na miundombinu ya barabara  na mitaro ambayo ni kero kwa wananchi.

Kwa upande wake katibu wa Siasa na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Katavi, Jackson Lema ameelekeza lawama kwa wakala wa barabara vijijini na mjini -Tarura na kuitaka kujitathimini katika kipindi hiki cha mvua ambacho barabara nyingi Mkoani Katavi hazipitiki.