Rubani wa Atcl awataka vijana nchini kuwa wazalendo

0
851

Rubani mzawa wa Shirika la Ndege Nchini Tanzania-Atcl raymond Musingi aliyerusha ndege aina ya Airbus 220 Dash 300 kutoka Canada hadi Tanzania amewataka vijana wa Kitanzania wenye nia ya kusomea fani hiyo kujituma katika masomo ya sayansi huku wakitanguliza uzalendo kwa taifa lao.

Musingi amesema hayo mapema asubuhi ya leo katika kipindi cha Jambo Tanzania kinachorushwa na Tbc One wakati akielezea ubora wa ndege mpya zilizonunuliwa na serikali ya Tanzania.

Aidha Capten Musingi amewaomba marubani wenzake kutumia fursa ya ndege za Atcl kuwaonesha abiria vivutio vya utalii wawapo angani ikiwemo mlima Kilimanjaro ili kuvutia watalii wengi kuja nchini.

Musingi amesema ndege aina ya Airbus 220 Dash 300 zimetengenezwa kwa teknolojia  mpya inayeoendana na mahitaji ya sasa katika usafiri wa anga.