Rais Magufuli ashiriki ibada maalum kumuombea Baba wa Taifa

0
2188

Rais John Magufuli na mke wake Mama Janeth Magufuli wameungana na waumini wengine katika Ibada maalum ya kumuombea Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Ibada hiyo imefanyika katika Kanisa la Mtakatifu Petro Oysterbay jijini Dar es salaam ikiwa ni miaka 19 tangu kifo cha Baba wa Taifa.

Mara baada ya Ibada hiyo, Rais Magufuli na mke wake Mama Janeth walimtembelea Mjane wa Baba wa Taifa, – Maria Nyerere nyumbani kwake Msasani jijini Dar es salaam.