Polisi kusaka waganga wa jadi

0
2232

Jeshi la Polisi mkoani Mwanza limetangaza kuanza msako dhidi ya waganga wa jadi wanaojihusisha na upigaji ramli chonganishi.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Mwanza, Jonathan Shana ametangaza msako huo kufuatia ongezeko la mauaji hususani ya wanawake yanayodaiwa kusababishwa na imani za kishirikina.

Kamanda Shana ametangaza msako huo alipokutana na wakuu wa polisi, wakuu wa upelelezi wa wilaya na wakuu wa vituo vya polisi mkoani humo.

Amesema msako huo utahusisha pia wanaotoa vibali kwa waganga hao huku akitangaza kiama kwa maofisa na askari polisi wanaodaiwa kuwabambikizia kesi wananchi.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Mwanza amewataka askari polisi kujiepusha na vitendo vya rushwa.