Mwili wa Annan waagwa Accra

0
2307

Mwili wa aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Kofi Annan unaagwa leo katika mji mkuu wa Ghana, Accra.

Mwili wa Annan uliwasili Jumatatu jioni katika uwanja wa ndege wa kimataifa ulioko mjini Accra ukitokea nchini Uswisi. Mazishi rasmi ya Annan yanatarajiwa kufanyika siku ya Alhamis wiki hii.

Annan alifariki dunia tarehe 18 Agosti mwaka huu baada ya kuugua kwa muda mfupi.

Amefariki dunia nchini Uswisi akiwa na umri wa miaka 80 .