Mnada wa mifugo Pugu Mnadani kuhamishwa

0
2369

Serikali imewaruhusu wakazi wa Pugu Mnadani eneo la Bangulo jijini Dar es salaam kuendelea kuishi katika eneo hilo, na hivyo kumaliza mgogoro wa ardhi wa muda mrefu katika eneo hilo.

Msimamo huo umetolewa leo na mawaziri kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Luhaga Mpina na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi wakati wa mkutano na wananchi wanaoishi eneo hilo, ili kumaliza mgogoro.

Waziri Mpina amesema serikali imeamua kuwamilikisha eneo hilo wananchi na kwamba itatafuta eneo lingine la kuweka mnada.

Naye waziri Lukuvi amewataka wakazi hao kurasimisha maeneo yao.

Awali Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda alisema lengo lake ni kumaliza migogoro ya ardhi katika jiji la Dar es salaam ndani ya mwaka huu.

Eneo la Bangulo lililoko wilayani lipo chini ya umiliki wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi ambayo iliwamilikisha Tanganyika Parkers mwaka 1939 na kufanywa kuwa eneo la mnada na kuhifadhi Mifugo.