Mkutano wa wakuu wa EAC waendelea Arusha

0
1268

Mkutano wa Ishirini wa kawaida wa Wakuu wa nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki unaendelea na kikao chake cha ndani  jijini Arusha.

Miongoni mwa Marais wanaoshiriki katika mkutano huo ni Dkt John Magufuli wa Tanzania, Uhuru Kenyatta wa Kenya, Yoweri Museveni wa Uganda na Paul Kagame wa Rwanda.

Habari kutoka jijini Arusha zinasema kuwa nchi za Burundi na Sudan Kusini zimetuma wawakilishi katika mkutano huo.

Mwenyekiti wa Baraza la Mawaziri la nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Dkt Ally Kivejinja amesema  kuwa kikao hicho kitajadili agenda mbalimbali zenye maslahi kwa nchi wanachama ikiwemo kuimarisha ushirikiano na usalama.