Byakanwa ahoji utendaji wa TARURA Mtwara

0
1196

Mkuu wa mkoa wa Mtwara Gelasius Byakanwa amesema haridhishwi na utendaji kazi wa Wakala wa Barabara Vijijini na Mijini – TARURA – mkoani humo ambao amewatuhumu kufanya kazi kwa kukurupuka bila ofisi yake kupewa taarifa.

Byakanwa ametoa kauli hiyo alipokuwa anazungumza kwenye kikao cha Bodi ya Barabara na kusema amelazimika kuunda Tume kuchunguza barabara zote za wilaya ya Mtwara ambazo hazipitiki na kuleta adha kwa wananchi.

Ubovu wa baadhi ya barabara katika manispaa ya Mtwara Mikindani na Halmashauri ya mji wa Nanyamba wilaya ya Mtwara umekuwa ukilalamikiwa na wakazi wa maeneo hayo mara kwa mara.

Baadhi ya wadau wa kikao hicho wameomba TARURA kushirikisha ofisi za Halmashauri kazi wanazofanya ili kuondoa mkanganyiko.