Ajali yasababisha vifo vya watu watatu

0
2361

Watu Watatu wamekufa papo hapo na mmoja kujeruhiwa katika ajali ya barabarani iliyohusisha magari mawili katika eneo la Hedaru – Kadama wilayani Same mkoani Kilimanjaro.

Kamanda wa polisi wa mkoa wa Kilimanjaro Hamis Issah amewataja watu waliokufa katika ajali hiyo kuwa ni Simon mbaga ambaye ni dereva wa gari aina ya scania, Ramadhan Jumanne dereva wa gari aina ya Kenta na mwingine ambaye ametambulika kwa jina moja la Mbongo.

Majeruhi katika ajali hiyo ni Said Tumaini ambaye amepatiwa matibabu katika hospitali ya wilaya ya Same na kuruhusiwa