Marekani na Uturuki zaanza mazungumzo kuhusu usalama

0
1043

Ujumbe wa Idara ya Ulinzi nchini Marekani umewasili mjini Ankara nchini Uturuki kwa ajili ya mazungumzo ya usalama baina ya mataifa hayo mawili.

Wachunguzi wa siasa za Magharibi wamesema miongoni mwa mambo ambayo pande hizo mbili zinatarajia kujadiliana ni pamoja na kurejeshwa nchini Uturuki, mhubiri maarufu wa dini ya Kiislam Fatullah Gullan, anayeishi nchini Marekani.

Serikali ya Uturuki imekuwa ikimtuhumu mhubiri huyo wa dini, mwanasiasa na mfanyabiashara maarufu, kuhusika na jaribio lililoshindwa la mapinduzi ya serikali ya Uturuki hata hivyo Gullan amekuwa akikanusha tuhuma hizo na kusema zimesababishwa kisiasa.

Nchi hizo mbili zinaangalia kama kuna uwezekano wa Marekani kumrejesha Gullan nchini Uturuki ili akabiliane na kesi ya uhaini inayomkabili.