AfDB kuangalia miradi zaidi ya kuwekeza Tanzania

0
2325

Waziri wa Fedha na Mipango Dkt Phillip Mpango amesema kuwa Tanzania ni miongoni mwa nchi chache Wanachama wa Benki ya Maendeleo ya Afrika(AfDB) zinazonufaika na miradi mbalimbali ya maendeleo inayofadhiliwa na benki hiyo.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam Dkt Mpango amesema kuwa katika kuelekea uchumi wa viwanda, miradi kadhaa ya maendeleo inafadhiliwa na benki hiyo kwa gharama ya zaidi ya shilingi trilioni Nne.

Katika mkutano huo na waandishi wa habari Dkt Mpango alifuatana na Mwakilishi wa Marekani katika Benki ya Maendeleo ya Afrika, – Steven Dowd ambaye yupo nchini kwa lengo la kuangalia na kufanya tathmini ya aina ya miradi itakayoweza kutekelezwa benki hiyo.

Akiwa hapa nchini, pamoja na mambo mengine Dowd atatembelea vivutio mbalimbali vya utalii.