CHALAMILA : HAKUWEZI KUWA NA UHABA WA MAFUTA DAR

0
296

Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila amesema mkoa huo una hifadhi ya kutosha ya mafuta kutokana na wawekezaji kupewa kipaumbele katika kuwekeza mkoani humo.

Chalamila amesema hayo alipofanya ziara katika ofisi za Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) zilizopo Mikocheni, Dar es Salaam na kuongeza kuwa mkoa wa Dar es Salaam hautakutana na
changamoto ya uhaba wa mafuta kwa kuwa kuna uwekezaji mkubwa uliofanywa na Wafanyabiashara wa mafuta.

Chalamila amewahakikishia Wananchi wa mkoa wa Dar es Salaam kuwa mkoa huo ni salama na vyombo vya ulinzi viko imara kuhakikisha mkoa huo upo shwari wakati wote.