Watanzania watakiwa kuiunga mkono serikali

0
1196

Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam, – Paul Makonda ametoa wito kwa Watanzania wote kuendelea kuunga mkono jitihada zinazofanywa na serikali za kuiletea nchi maendeleo na kuifanya iweze kujitegemea.


Makonda ametoa kauli hiyo jijini Dar es salaam wakati wa mkutano wa wachimbaji wadogo wa madini, wafanyabiashara na wadau wa sekta ya madini.


Mkuu huyo wa mkoa wa Dar es salaam ametumia mkutano huo kuwaomba Watanzania wote kuendelea kuwa wazalendo hasa katika kuitetea nchi yao mahali popote walipo na wale wenye nia ya kuitangaza nchi vibaya kuacha kufanya hivyo.


Amempongeza Rais John Magufuli na serikali yake kwa kazi nzuri ya kuliletea Taifa maendeleo ikiwemo ile ya kuboresha miundombinu ya aina mbalimbali.


Ufunguzi wa mkutano huo wa wachimbaji wadogo wa madini, wafanyabiashara na wadau wa sekta ya madini pia umehudhuriwa na Rais John Magufuli, Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan, viongozi mbalimbali wa serikali, siasa pamoja na wale wa kidini.