Wanamichezo, Wasanii kuombeleza

0
2228

Waziri wa habari, utamaduni, sanaa na michezo Dkt Harrison Mwakyembe ameagiza mabaraza ya michezo na sanaa ya taifa na mashirikisho husika kuendesha shughuli zao kwa kuzingatia taifa liko kwenye maombolezo.

Waziri Mwakyembe amewataka wachezaji na watazamaji wa michezo mbalimbali kusimama kwa dakika moja kabla ya michezo kuanza ili kuwaombea marehemu na majeruhi wa ajali ya kivuko cha mv nyerere iliyotekea tarehe 20 septemba mwaka huu katika ziwa viktoria.

Pia amevitaka vyombo husika vya michezo kuhakikisha kila mchezaji anafunga kitambaa cheusi kwenye mkono, ishara ya wanamichezo kuomboleza msiba huo.

Aidha Waziri huyo wa habari, utamaduni, sanaa na michezo ameliagiza baraza la sanaa la taifa lihakikishe kuwa wamiliki wa kumbi za wazi za starehe wanadhibiti kelele za shamrashamra na upigaji muziki usiozingatia kipindi cha maombolezo kitakachohitimishwa septemba 24 mwaka huu.