Wakala wa barabara watakiwa kujenga haraka barabara mkoani Pwani

0
873

Bodi ya Barabara Mkoa wa  Pwani imewaagiza Wakala wa Barabara Vijijini na Mijini -Tarura kujenga haraka barabara ambazo zinafungua maeneo yote yaliyotengwa kwa ajili ya uwekezaji.


Agizo hilo limetolewa Mjini Kibaha na Mwenyekiti wa Bodi hiyo Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Evarist Ndikilo wakati akifungua kikao cha bodi  hiyo cha kujadili na kupitisha bajeti ya fedha zitakazitumika kujenga miradi ya barabara  katika kipindi cha mwaka 2019/2020..

Pia amewataka Wakala wa Barabara Vijijini na Mijini -Tarura kufungua barabara  zote zinazoenda katika maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya uwekezaji na kutoa agizo kwa Wakala wa Barabara nchini -Tanroads pamoja na Tarura kuhakikisha barabara  wanazojenga zinaendana na kiasi cha fedha kilichotengwa.


Kwa upande wake Meneja wa Wakala wa Barabara  Mkoa wa Pwani, Yudas Msangi amesema katika kipindi cha mwaka 2019/2020 zaidi ya Shilingi Bilioni arobaini ma sita zimetengwa kutekeleza miradi mbalimbali ya barabara  ikiwemo upanuzi wa Daraja la Mto Wami.

Naye Mbunge wa Jimbo la Kibaha Mjini, Silvestry Koka ameishukuru serikali kwa kuanza kujenga barabara za lami katika kitovu cha mji huo.