Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Dakta Mary mwanjelwa amewaagiza makamishna wa tume ya utumishi wa umma kuanza kuwashughulikia viongozi wanaotumia madaraka vibaya kwa lengo la kurudisha nyuma sekta ya utumishi wa umma.
Akifungua mafunzo elekezi kwa makamishna hao wateule Dakta Mwanjelwa amesema wakati serikali ikiendelea na mkakati wake wa kuleta mapinduzi ya uchumi wa viwanda lazima watumishi wa umma wafahamu kuwa wanahitajika kuwa wabaunifu kiutendaji ili kufikia malengo hayo kwa kuchapa.
Dakta Mwanjelwa pia amewataka makamishna hao kutumia nafasi yao kutatua changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta ya umma ikiwa ni pamoja na kutatua changamoto za waajiri na wafanyakazi kwa wakati.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Tume a Utumishi wa Umma Jaji Mstaafu Dakta Stephen bwana amesema kuwa atahakikisha matatizo yanayoikabili sekta ya umma yanapatiwa ufumbuzi wa haraka .
Tume ya Utumishi wa Umma iliyoteuliwa hivi karibuni na Rais John Magufuli itakuwa na majukumu ya kushughulikia kero zinazoikabili sekta ya umma .