Taa za sola pamoja na jenereta ruksa

0
1295

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Luhaga Mpina ameagiza wavuvi wanaotumia taa za sola pamoja na jenereta kwa ajili ya shughuli za uvuvi wasikamatwe mpaka hapo utakapoandaliwa utaratibu mwingine.

Waziri Mpina ametoa agizo hilo Bungeni jijini Dodoma wakati wa kipindi cha maswali na majibu.

Amesema kuwa Julai Mosi mwaka huu, serikali itatoa maelekezo zaidi kuhusu matumizi ya vifaa hivyo na kwamba haikusudii kuzuia matumizi ya taa hizo za sola pamoja na jenereta kwa Wavuvi kwenye maeneo mbalimbali nchini.  

Naye Naibu Waziri wa Afya , Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt Faustine Ndugulile ameliambia Bunge kuwa serikali ina mpango wa kuweka huduma ya kipimo cha  CT SCAN katika hospitali za mikoa mbalimbali nchini ili kurahisisha upatikanaji wa huduma hiyo.

 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, – January  Makamba naye amepata nafasi ya kujibu swali bungeni Ijumaa Februari Mosi na kuwataka Wakazi wa Zanzibar kuandika anwani sahihi pindi wanapoomba na kupata ajira katika taasisi za Muungano, lengo likiwa ni kufahamu uwiano wa watendaji katika taasisi hizo kwenye pande zote za Muungano.