Marioo kinara chati ya muziki TBC FM

0
6478

Mwanamuziki Omary Mwanga almaarufu Marioo ameendelea kuing’ang’ania nafasi ya kwanza katika chati ya Top 20 za muziki TBC FM kwa wiki tatu mfululizo.

Wimbo wake wa Mi Amor ambao bado umeendelea kuwa zeze masikioni mwa wengi ndio ambao unamkalisha Marioo kwenye kiti hicho cha wakali wa muziki.

Katika kumi bora nafasi ya pili hadi kumi wapo; 10. Zuchu- Mwambieni, 9. Camila Cabello – Bam Bam, 8.Shilole – Mama Ntilie, 7. Linex feat Barakah Da Prince – Baby Mama, 6.Nandy feat Bilnass & Mr.Easi – Party, 5. Goya Menor ft Nektunez – Ameno Amapiano, 4. Mrisho Mpoto feat Mbosso -Tausi, 3. Diamond – Nawaza, na 2. Ali Kiba-Utu.

Orodha nzima imewekwa kwenye picha.