Kiwanda kipya cha Sukari kujengwa Kilombero

0
1049

Kiwanda cha sukari cha Kilombero  kilichopo mkoani Morogoro kinakusudia kujenga kiwanda kikubwa kitakacho gharamu kiasi cha shilingi  bilioni 650  ili kuongeza uzalishaji wa sukari kutoka tani milioni 1.2 zilizopo sasa hadi kufikia tani  milioni  2.4 kwa mwaka.

Akizungumza katika mkutano wa wadau uliokuwa na lengo la kujadili upanuzi wa kiwanda hicho, Mkurugenzi wa mahusiano wa kiwanda hicho Joseph  Rugaimkamu  amesema ujenzi wa kiwanda hicho kipya utaenda sambamba na upanuzi wa mshamba ya miwa ya kiwanda pamoja na wakulima wan je  ili kukidhi mahitaji ya sukari katika soko la ndani na nje ya nchi.

Amesema ujenzi wa kiwanda hicho  utasaidia kuongeza upatikanaji wa sukari katika soko la ndani na nje ya nchi.

Kwa upande wake Mkuu wa mkoa wa Morogoro Dakta  Stephen Kebwe amezitaka halmashauri za Kilosa na Kilombero kushiriki kikamilifu ili kufanikisha mchakato wa  utekelezaji wa maagizo ya serikali ya awamu ya tano ya kuhakikisha sukari iliyopo nchini inajitosheleza .