DKT. MWINYI : TUTAENDELEA KUTIMIZA TULIYOYAAHIDI

0
267

Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar,
Rais wa Zanzibar Dkt.Hussein Mwinyi amesema ataendelea kutimiza ahadi alizowaahidi Wananchi na kutekeleza ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020-2025.

Dkt.Mwinyi ameyasema hayo alipokutana na Wenyeviti wa Chama cha Mapinduzi wa mikoa ya Tanzania Bara na Zanzibar waliofika Ikulu Zanzibar leo Agosti 30, 2023.

Aidha, Dkt. Mwinyi amempongeza Mwenyekiti wa CCM Taifa Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutoa mialiko kwa Wenyeviti hao kuhudhuria Tamasha la Kizimkazi mwaka huu.

Naye Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa, Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Tabora, Hassan Wakasuvi akizungumza kwa niaba ya Wenyeviti hao wa CCM wa mikoa amempongeza Rais Mwinyi kwa mabadiliko ya maendeleo yaliyofanyika Zanzibar chini ya uongozi wake na kuendelea kutekeleza vema ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020-2025.