Ubelgiji wataka ulinzi zaidi wa mazingira

0
1555

Maelfu ya raia wa Ubelgiji wameandamana katika mitaa mbalimbali ya mji mkuu wa nchi hiyo Brussels wakitaka kuwekwa kwa mikakati zaidi ya kulinda mazingira.

Raia hao wameandamana wakati ambapo mkutano mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mazingira (COP 24) ukianza rasmi katika mji wa Katowice nchini Poland

Polisi nchini Ubelgiji wamesema kuwa karibu watu elfu 65 wameandamana mjini Brussels  wakiitaka serikali ya nchi hiyo na za nchi  nyingine za Ulaya kuweka hatua kali za kulinda utoaji wa gesi ya ukaa.

Wamesema kuwa ni kwa njia hiyo tu ulimwengu utaweza kupunguza kiwango cha joto duniani kwa Sentigredi 1.5 na kuyafikia malengo ya mkataba wa mazingira wa Paris wa mwaka 2015.

Maandamano kama hayo kuhusiana na masuala ya mazingira yamefanyika kwenye miji mingine ya nchi za Ulaya ikiwa ni pamoja na Berlin na Cologne nchini Ujerumani.