Trump ashinda uteuzi mgombea Urais Republican

0
574

Donald Trump ameshinda uteuzi wa kuwa mgombea wa Urais wa Marekani kupitia chama cha Republican baada ya kupata ushindi wa asilimia 59.8 ya kura dhidi ya Nikki Haley aliyepata asilimia 39.5 katika jimbo la South Carolina.

Baada ya ushindi huo wa Trump, kwa sasa anategemea kukutana tena na mrithi wake ambaye ni Rais Joe Biden wa Marekani.

Kwa upande wake Haley ambaye aliwahi kuwa Gavana maarufu wa jimbo la South Carolina kwa mihula miwili, amempongeza Trump kwa ushindi huo.