Rais wa Benki ya dunia aatangaza kujiuzuru

0
886

Rais wa Benki ya Dunia, Jim Yong Kim ametangaza kuwa atajiuzuru mwezi ujao, ikiwa ni miaka mitatu kabla ya muhula wake kumalizika mwaka 2022.

 Kim ambaye anajiunga na kampuni binafsi inayoangazia uwekezaji katika mataifa yanayoendelea, amesema imekuwa ni heshima kubwa kwake kuiongoza taasisi hiyo muhimu.

Afisa mkuu wa benki ya dunia, Kristalina Georgieva, atachukua nafasi ya rais wa mpito baada ya kim kuondoka Februari mosi.

Kim alianza kipindi chake cha pili kama rais wa benki ya dunia, Julai, 2017.