Maafisa usalama Marekani wapongezwa

0
1822

Aliyekuwa mgombea wa kiti cha urais nchini Marekani katika uchaguzi mkuu wa nchi hiyo uliopita Hilarry Clinton amewapongeza maafisa usalama nchini humo kwa kubaini milipuko iliyokuwa imelengwa kumuangamiza.

Hillary amesema kuwa maafisa usalama nchini humo wamefanya kazi kubwa ya kuokoa maisha yake na ya familia yake baada ya kutumiwa kifurushi ambacho kilibainika kuwa na vitu vyenye milipuko.

Idara ya usalama nchini Marekani pia imethibitisha kifurushi kingine alichotumiwa Rais wa zamani wa nchi hiyo Barack Obama pamoja na bilionea mmoja nchini humo, vyote vilikuwa na vitu vyenye milipuko.

Kifurushi kingine kama hivyo kilitumwa katika ofisi za kituo cha televisheni cha CNN nchini Marekani.

Rais Donald Trump wa Marekani amewalaumu wale wote waliohusika na matukio hayo na kusema kuwa hayawezi kuvuruga amani na demokrasia nchini humo.