Korea Kaskazini kuzima moja ya mitambo yake ya nyuklia

0
2289

Rais wa Korea Kusini Moon Jae-in amesema kuwa Rais Kim Jong-un wa Korea Kaskazini amekubali kuzima moja ya mitambo yake mikubwa ya nyuklia na majaribio ya makombora.

Amesema kuwa Rais Kim amekubali kuzima kabisa mtambo huo unaojulikana kama Tongchang-ri, tukio litakaloshuhudiwa na wataalam wa nyuklia kutoka mataifa mbalimbali.

Moon amesema kuwa baada ya mkutano wao wa tatu katika mji wa Pyongyang, wamekubaliana masuala mbalimbali yanayohusu mpango wa nyuklia wa Korea Kaskazini.

Kim mwenyewe amesema kuwa mazungumzo yao yamekwenda vizuri na makubaliano waliyofikia yana faida kubwa kwa pande zote mbili na hata mataifa mengine.

Kwa mujibu wa Rais huyo wa Korea Kaskazini, atafanya ziara Korea Kusini hivi karibuni ikiwa ni ziara ya kwanza kwa kiongozi wa Korea Kaskazini katika taifa hilo.